Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

2 4 /

U O N G O F U & W I T O

a. Mungu alijitambulisha moja kwa moja na Neno katika nafsi ya Yesu Kristo, Yohana 1:1-2.

b. Yesu Kristo ni Neno la Mungu aliyefanyika mwili (Yohana 1:14). (1) Kudhihirishwa kwa Mungu katika mwili ulimwenguni. (2) Ufunuo maalum kwa ajili ya wanadamu wote kuuona.

c. Hakuna mtu mwingine au kitu kinachoweza kutangaza utukufu wa Mungu kama Neno aliyefanyika mwili. (1) Yohana 1:18 (2) 1 Yohana 1:1-3

1

d. Jina la Yesu linaloitwa waziwazi “Neno la Mungu,” Ufu. 19:13.

C. Aina mbili muhimu za Neno la Mungu: Neno-kauli na Neno-mtu.

1. Aina ya 1: Neno la “kauli” la Mungu – Neno la Mungu lililoandikwa kwa uvuvio

a. Neno la Mungu lililovuviwa, Maandiko ya Kiebrania ya Agano la Kale, na Maandiko ya Kikristo ya Agano Jipya.

b. Maktaba, iliyovuviwa na Roho na kuandikwa kwa zaidi ya miaka 1500, na waandishi 40.

2. Aina ya 2: Neno la Mungu “mtu” - Bwana Yesu Kristo

Made with FlippingBook flipbook maker