Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi
2 6 /
U O N G O F U & W I T O
6. Kuna uhusiano gani kati ya uumbaji wa ulimwengu na Neno la Mungu? Nini maana ya maneno ya Kilatini, « ex nihilo ,» na dhana hii inahusiana vipi na mada ya Mungu ya uumbaji? 7. Maandiko yanasema nini kuhusu uhusiano wa uumbaji wa Mungu wa ulimwengu wote mzima na Logos , au Neno la Mungu (yaani, Yesu Kristo)? 8. Nini maana ya “ufunuo wa jumla”? Je, ni njia zipi mahususi ambazo Mungu amejidhihirisha kwa ujumla kwa wanadamu wote? 9. Nini maana ya maneno “ufunuo maalum?” Je, ni njia zipi mahususi ambazo kwazo Mungu amejidhihirisha kwa watu mahususi kwa nyakati na mahali maalum? 10. Je, kuna tofauti gani kati ya Neno la Mungu la “kauli” na Neno “mtu”? Je, dhana hizi zinahusiana vipi? Je, moja inachukua nafasi ya kwanza (yaani, ni muhimu zaidi) kuliko nyingine? Eleza.
1
Neno Linaloumba Sehemu ya 2
Mch. Dkt. Don L. Davis
Neno la Mungu ni njia ambayo kwayo Roho Mtakatifu anaumba maisha mapya ndani ya wale wanaoamini. Kwa hiyo, kupokea Neno na kudumu katika Neno hili la Mungu lililopandikizwa ndani yetu ni ishara ya kweli ya ufuasi na kufanywa wana wa kweli katika familia ya Mungu. Kama watakatifu wa Mungu, tunapokea Neno la Mungu pamoja katika jamii yake ya agano. Hatimaye, kwa sababu ya kutegemeka kwa Neno, ndilo pekee linaloweza kututangazia kusudi kuu la ulimwengu ulioumbwa, ambalo ni utukufu wa Mungu Mwenyezi. Lengo letu la sehemu hii ya pili ya Neno Linaloumba ni kukuwezesha kuona kwamba: • Neno la Mungu limetiwa uzima wa Mungu mwenyewe, na kwa hiyo, hakuna hali ya kiroho au dini ya kweli inayowezekana bila nguvu zinazotoa uhai za Neno la Mungu. Mungu huumba maisha mapya kwa waamini kupitia Neno lake, likiangaziwa na Roho Mtakatifu.
Muhtasari wa Sehemu ya 2
Made with FlippingBook flipbook maker