Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi
/ 2 7
U O N G O F U & W I T O
• Ishara ya kweli ya ufuasi ni kukaa ndani ya Neno na kuendelea katika upokeaji endelevu wa Neno la Mungu kama roho na kweli. Ukomavu wa kiroho unahusishwa moja kwa moja na kusikia na kutii Neno la Mungu katika Kanisa. • Kwa sababu ya mamlaka yake isiyoweza kukosea, ni Neno la Mungu pekee linaloweza kutupatia kusudi kuu la ulimwengu ulioumbwa, ambalo ni kumletea Mungu heshima na utukufu katika mambo yote.
I. Neno la Mungu Limetiwa Uzima wa Mungu Mwenyewe, na Kwa sababu hiyo Linaumba Maisha Mapya ndani ya Wale Wanaoamini.
Muhtasari wa Sehemu ya 2 ya Video
1
A. Neno hujenga maisha ya kiroho kama matokeo ya imani katika kazi ya Yesu Kristo.
1. Neno la Mungu ni la msingi katika kuumba maisha mapya ya kiroho ndani ya mwamini.
a. Yakobo 1:18
b. Yakobo 1:21
2. Neno la Mungu ndilo chombo, mbegu isiyoharibika, ambayo huzaa maisha mapya ndani yetu kupitia imani yetu katika Yesu Kristo, 1 Pet. 1:22-23.
3. Injili inayomhusu Yesu na Ufalme wake haitokani na mwanadamu, bali “yenyewe ni Neno la Mungu,” 1 Thes. 2:13.
B. Uhai wa kiroho unaumbwa na Neno la Mungu lililo hai: tunaishi kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.
Made with FlippingBook flipbook maker