Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi
/ 3 7
U O N G O F U & W I T O
jambo lolote linalofundishwa katika Maandiko. Mchungaji ameweka wazi kwamba haya ni maoni yake tu kuhusu Maandiko, lakini ni mwalimu mwenye nguvu na wengi wanaona mawazo yake kuwa yenye mantiki. Mchungaji ni kiongozi wa kibiblia, mwalimu mzuri wa Kikristo, na ndugu mnyenyekevu katika Kristo. Dada huyu anapaswa kufanya nini katika hali hii?
Kukana Imani?
Katika darasa la sayansi shuleni, mmoja wa wanafunzi katika kikundi cha vijana analazimika kuandika andiko la muhula kuhusu nadharia ya mageuzi. Mwanafunzi huyu huyu amekuwa akijifunza kanisani jinsi Mungu alivyoumba ulimwengu kupitia Neno lake, na kimahususi zaidi, kupitia Yesu Kristo. Anayaamini Maandiko, kwamba fundisho la Biblia kuhusu uumbaji ni sahihi, na bado Biblia haionekani kuzungumzia masuala yote anayokabiliana nayo darasani kuhusu sayansi. Hataki kugeuza darasa lake la sayansi kuwa kikundi cha mazungumzo ya kidini, lakini anatatizika kutafuta njia ya kuzungumzia maoni ya Biblia kuhusu uumbaji katika darasa lake la sayansi katika shule ya sekondari. Ikiwa ndugu huyo mchanga angekujia ili kupata ushauri, ungemshauri afanye nini au asifanye nini? Katika moja ya ushemasi wa kanisa kumetokea mabishano makubwa katika kipindi cha mafunzo ya Biblia ya nyumbani kuhusu tafsiri gani za Biblia zinafaa kutumiwa. Kikundi kimoja cha waamini wazee kimedai kwamba Biblia pekee inayopaswa kutumika katika kundi hilo ni Biblia ya King James, tafsiri iliyothibitishwa na ya kweli ambayo kwa muda mrefu imeheshimiwa na kuthaminiwa kanisani. Kundi la vijana wanasisitiza kutumia baadhi ya tafsiri za “kisasa”, kwa sababu wanaona ni rahisi sana kusoma na kukariri. Kwa wale wa kundi la watu wazima, mstari unaposomwa kutoka katika tafsiri mpya zaidi, wanahisi kana kwamba maana nzima ya mstari huo imebadilika. Pande zote mbili zinajua kwamba Biblia haikuandikwa awali katika Kiingereza, lakini hakuna hata mmoja katika makundi yote mawili anayeelewa Kiebrania au Kiyunani. Kama mchungaji, unawezaje kutatua tatizo hili katika ushamasi huu? Neno la Mungu kwa mujibu wa King James wa Uingereza
2
1
3
Unamhitaji Roho Mtakatifu
Baada ya kusikia fundisho kwenye televisheni lililosema kwamba hakuna mtu anayeweza kuielewa Biblia bila msaada wa Roho Mtakatifu, shemasi mmoja kanisani anahangaika sana kwa habari ya kutoelewa kwake Biblia. Ingawa
4
Made with FlippingBook flipbook maker