Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

/ 6 5

U O N G O F U & W I T O

* Ni njia gani zinazofaa tunazoweza kuwasaidia wengine kuelewa kwamba Yesu Kristo mwenyewe ndiye mada kuu na ujumbe mkuu wa Maandiko? Je, kuna jambo lolote linaloweza kuwa na nguvu ya kushawishi kiroho na lisiwe na uhusiano wa namna fulani na Yesu Kristo? Elezea jibu lako. * Kwa nini ni muhimu kuamini katika uadilifu na ukweli wa Mitume na manabii ili kuwa na msimao thabiti kwamba Maandiko ni ushahidi wa kweli na wenye kutegemeka wa kazi ya Mungu katika Kristo? * Kwa nini ni muhimu kwa mtu anayewahubiria waliopotea katika maeneo ya miji kuwa na uelewa sahihi juu ya uwezo wa Maandiko wa kuwathibitishia watu? Kwa heshima ya maendeleo ya tamaduni mbalimbali na ushirikiano kati ya dini mbalimbali katika jamii, umealikwa kwenda na kutoa maoni yako kuhusu “asili ya ukweli wa kidini katika jamii yenye mchanganyiko wa kiimani.” Kwa maneno mengine, katika jamii ambamo watu wake wanafuata na kuamini aina nyingi za dini, ina maana gani “kutafuta ukweli na kusema ukweli” kama mwamini Mkristo? Baadhi ya wenzako wanaamini unapaswa kwenda na kusema tu kwamba dini nyingine zote ni za uongo; Ukristo pekee ndio imani ya kweli, Kristo ndiye Bwana, na ndivyo ilivyo. Unataka kuwa wazi juu ya imani yako iwezekanavyo, wakati huo huo, ukiwa makini kuzingatia madhumuni ya tukio hilo, ambalo si kwa ajili ya kuhubiri bali umeitwa kutoa maoni yako. Ungewashirikishaje imani ya kibiblia katika muktadha huu, hasa kuhusu msimamo wa Ukristo kwamba Yesu ni wapekee na wa tofauti kati ya wengine wote wanaodai kunena kwa niaba ya Mungu? Mmoja wa vijana wakomavu kanisani anaomba kuzungumza nawe kuhusu mada ya “dhambi.” Kama mfanyakazi wa kijamii aliyeajiriwa serikalini, ameambiwa mara kwa mara kutoruhusu imani yake binafsi ya kidini kuingilia kazi yake ya kutoa ushauri na taarifa kwa «wateja» wake, ambao wengi wao ni wafanyakazi kwenye miradi ya umma na wanahitaji sana kumjua Kristo. Moja ya sababu kuu za vikwazo hivi ilitokea hivi majuzi katika mjadala ambapo msimamizi wake alitilia shaka kabisa dhana ya «dhambi.” Katika kutetea msimamo wake dhidi ya dhambi, msimamizi huyo alisema kwamba “dhambi” ni dhana tu ya vikundi fulani vya kidini vyenye nia ya kulazimisha maadili yao finyu juu watu wengine. Hakuna mtu Je, Ukristo ni Dini ya Kipekee kati ya Dini Zote? Dhambi ni Kitu Gani Hasa?

MIFANO

2

1

ukurasa 188  17

2

Made with FlippingBook flipbook maker