Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

/ 7 9

U O N G O F U & W I T O

2. Baada ya Msalaba , Neno linalogeuza ni Injili ya Yesu Kristo.

a. Yesu ni Mwanakondoo wa Mungu aichukuaye dhambi ya ulimwengu (yaani, kwa dhabihu yake Msalabani), Yoh. 1:29.

b. Yesu alifuta kumbukumbu ya deni letu pale msalabani, pamoja na madai yote ya kisheria dhidi yetu, Kol. 2:14-15.

c. Dhabihu ya Yesu msalabani inatosha kabisa kuwa dhabihu kwa ajili ya dhambi, Ebr. 10:11-13.

3. Yesu alikufa badala ya wanadamu wenye dhambi, akibeba katika mwili wake hatia na mashutumu yetu, 1 Pet. 2:24.

3

4. Neno linashuhudia kuhusu upeo wa kazi iliyokamilika ya Mungu katika Yesu Kristo.

a. Kazi yake ilikuwa kwa ajili ya ulimwengu wote. (1) Yohana 3:16 (2) Ebr. 2:9

b. Kazi yake pia ilikuwa kazi ya usuluhishi na ukombozi kwa wanadamu wote, 1Tim. 2:5-6.

c. Kazi yake ilikuwa kazi ya upatanisho kwa wanadamu wote. (1) 2 Kor. 5:18-21 (2) 1 Yohana 2:2

B. Uongofu unahusu Neno, si matendo.

Made with FlippingBook flipbook maker