Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

/ 8 9

U O N G O F U & W I T O

D. Ishara ya mwisho ya ndani ya uongofu inahusiana na uwezo wa kumsikiliza Yesu Kristo na kumfuata . Waamini wapya wanaitambua na kuifuata sauti ya Mwokozi.

1. Wale wanaomjua wataisikiliza sauti yake, wala hawataifuata sauti ya wageni (Yohana 10:1-6).

2. Ushirika na Mungu unategemea kuendelea kutembea katika nuru , na kupokea utakaso kupitia damu ya Yesu kwa ajili ya dhambi katika maisha ya mtu, 1 Yoh. 1:5-10.

3. Wale walio wa Mungu wanatamani kumfuata Mungu na kutafuta njia za kuitikia ipasavyo mapenzi yake yaliyonenwa na kufunuliwa, 1 Yohana 2:3-6.

3

II. Neno la Mungu Linazalisha Ndani ya Mkristo Ishara za Nje za Wokovu Ambazo Zinatoa Ushahidi wa Toba na Imani ya Kweli.

ukurasa 195  10

A. Uhusiano thabiti na utambulisho pamoja na Wakristo wengine – watu wa Mungu kama familia yake mpya na jamaa zake wapya.

1. Neno la Mungu ni mbegu inayozaa “kuzaliwa upya” katika familia ya Mungu .

a. Tusipozaliwa kutoka juu kwa “maji” na kwa Roho, hatuwezi kuingia katika Ufalme wa Mungu. (1) Yohana 1:12-13 (2) Yohana 3:5

b. Neno la Mungu ni “ mbegu ” na “ neno lililopandikizwa ” ambalo huzaa maisha mapya ndani yetu, Yakobo 1:18, 21.

Made with FlippingBook flipbook maker