Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

20

Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa

C. Tambua na uelewe wito wa Mungu kwa maisha yetu yote , pamoja na wito wake maalum kwa wale walioitwa kuandaa na kuwajenga watu wake.

1. Wito maalum wa Mungu na huduma tano za uwezeshaji katika Waefeso 4 : mitume, nabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu.

2. Wanaume na wanawake wa uchaguzi na ufunuo wa Mungu mwenyewe.

3. Karama za vipawa vitokanavyo na upaji na uwepo wa Mungu mwenyewe.

D. Bwana Mwenye Enzi Kuu juu ya ulimwengu wote anawaita watu kwake, na anawaita ili wawe wawakilishi wake.

1. Alikusudia wito huu kabla ulimwengu haujaanza, 2 Tim.1:9 (SRUV) – ambaye alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, si kwa kadiri ya matendo yetu sisi, bali kwa kadiri ya makusudi yake mwenyewe na neema yake. Neema hiyo tulipewa katika Kristo Yesu kabla ya wakati kuanza.

2. Ni wito shirikishi wa kimbingu, Ebr. 3:1 – Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo yetu, Yesu.

3. Kwa hiyo, wajibu wetu ni kuishi katika namna itakayofanya wito na uteule wetu kuwa thabiti katika mioyo yetu wenyewe , 2 Pet: 1:10 – Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software