Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

Kipinidi cha 1 : Utangulizi

19

II. Wito Mmoja, Madhihirisho Mengi : Njia yenye Mitazamo Mingi katika Kujifunza Wito Halisi

Kwa hiyo twawaombea ninyi sikuzote, ili Mungu wetu awahesabu kuwa mmekustahili kuitwa kwenu, akatimiza kila haja ya wema na kila kazi ya imani kwa nguvu. ~ 2 Wathesalonike 1:11

Je, tunagunduaje wito wetu mahususi katika mwili wa Kristo?

A. Tambua na uelewe vipengele vya wito halisi wa Mungu

1. Wito wa Mungu kwa wokovu : wito halisi unaonyeshwa katika toba na imani kwa Bwana Yesu Kristo.

2. Wito wa Mungu kwa utakatifu : wito halisi unaoonyeshwa kwa kutengwa na Bwana kwa ajili ya kuwa milki yake, kwa kusudi, na furaha yake.

3. Wito wa Mungu kwa uhuru : wito halisi unaoonyeshwa katika ukombozi kutoka katika utumwa wa dhambi na dini ili kuingia katika maisha ya upendo thabiti kwa Mungu na kwa wengine.

4. Wito wa Mungu kwa jumuiya : wito halisi unaonyeshwa katika kufanyika sehemu ya jumuiya ya kiagano ya Mungu na kuiwakilisha jumuiya hiyo.

B. Tambua na uelewe majukumu ya wito wa Mungu

1. Wito wa Mungu kwa ajili ya kutumika : wito halisi unaonyeshwa katika kutumia karama, rasilimali, na fursa za mtu kulijenga Kanisa na kuvuna ulimwengu.

2. Wito wa Mungu wa kuteseka : wito halisi unaonyeshwa kwa utayari wa kujitolea, kupambana, na kuvumilia kwa gharama yoyote ili kutimiza mapenzi ya Mungu.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software