Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

18

Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa

a. Wito huo unajumuisha watu kutoka mataifa na rangi zote, 1 Kor. 1:24 – bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu.

b. Inahitaji mwangaza wa kiroho ili kuuelewa kikamilifu, Efe. 1:18 – macho ya mioyo yenu yatiwe nuru, mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo.

c. Ni lazima tujitahidi kuujua wito wetu ili tuweze kuenenda kama inavyoustahili , Efe. 4:1 – Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa.

d. Hatimaye, wito wetu utahusisha utukufu halisi wa Yesu Kristo , 2 The. 2:14 – aliyowaitia ninyi kwa injili yetu, ili kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo.

G. Asili isiyobadilika ya wito wa Mungu, Rum. 11:29 – Kwa sababu karama za Mungu hazina majuto, wala mwito wake.

1. Wito na karama za Mungu haziwezi kubatilishwa ( Mungu hatamwondolea mtu wake aliyemwita kazi ile aliyomwitia kufanya ).

2. Wito wa Mungu ndio suala la muhimu zaidi linaloamua mengine yote katika hali zote za kiroho na huduma (Isaya 11).

3. “Wito wa Mungu hauwezi kubatilishwa, si kwamba hauwezi kupingwa.”

Made with FlippingBook Digital Publishing Software