Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa
Kipindi cha 2 Wito wa Wokovu Kuelewa Wito Halisi kama Wito wa Wokovu
Rum. 8:28-30 Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye kwa kusudi lake. 29 Maana wale awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. 30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza. 2 The. 2:14 Aliyowaitia ninyi kwa injili yetu, ili kuupata utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo 1 Kor. 1:2 Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, wale waliotakaswa katika Kristo Yesu, walioitwa wawe watakatifu, pamoja na wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo kila mahali, Bwana wao na wetu. Flp. 3:14 Nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu
Je, tunaweza kujifunza nini katika kutazama vipengele hivi vya wito wa Mungu?
• Ni vipengele jumuishi kwa maana kwamba vinamgusa kila mtu ndani ya jumuiya ya kiagano (yaani, watu binafsi, familia, na watu wote) kwa ukamilifu, katika nyanja zote za maisha. • Vimeungamanishwa kwa maana ya kwamba vinaamua na kufafanua kila kitu kingine kinachohusishwa na utekelezaji wa wito wa Mungu. • Ni vya jumla kwa maana kwamba vinatumika kwa watu binafsi na familia zote kwa usawa, bila kujali wito fulani ambao Mungu anao kwa maisha yao binafsi.
I. Kuelewa Wito Halisi kama Wito wa Wokovu
Yesu ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme. Na Bwana wa ulimwengu wote anaamrisha kila mtu kumfuata. Wito wake kwa Petro na Andrea (Mt. 4:18-19) na kwa Yakobo na Yohana (Mt. 4:21) ulikuwa ni amri. “Nifuate” daima imekuwa amri, kamwe si mwaliko (Yohana 1:43). Yesu hakuwahi kumsihi mtu amfuate. Alikuwa wazi sana. Alimkabili mwanamke kisimani na uzinzi wake, Nikodemo na kiburi chake cha kiakili na Mafarisayo kwa kujiona kwao kuwa wenye haki. Hakuna anayeweza kutafsiri “. . . Tubuni, kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia” kama ombi (Mt. 4:17). Yesu aliamuru kila mtu aachane na mambo ya ubinafsi, aache dhambi yake na kumtii kabisa. Yule mtawala kijana tajiri alipokataa kuuza vitu vyote na kumfuata (Mt. 19:21) Yesu hakumkimbilia akijaribu kufanya mapatano ya kupata muafaka naye. Hakuwahi kushusha kiwango chake. Yesu alisema tu, “Mtu yeyote akinitumikia lazima anifuate . . .” (Yohana 12:26, NEN). . . . Basi ni lini unakuwa Mkristo, mwanafunzi wa Kristo? Unapopita mbele kuitikia wito wa muhubiri? Unapopiga magoti mbele ya madhabahu? Unapolia kwa dhati? Si lazima. Wafuasi wa awali wa Kristo walikuwa wafuasi walipomtii, wakati “walipoiacha mara moja mashua yao na baba yao, wakamfuata” (Mt. 4:22). Kutii amri ya Kristo, “Nifuate,” husababisha kujikana. Ukristo bila kujikana ni falsafa ya kufikirika tu. Ni Ukristo bila Kristo. ~ Keith Phillips. The Making of a Disciple . Old Tappan, NJ: Fleming H. Revell Company, 1981. uk. 16-17.
23
Made with FlippingBook Digital Publishing Software