Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

24

Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa

A. Ufafanuzi wa wito wa wokovu katika hadithi ya Kutoka

1. Wito maalum wa Musa, Kut. 3:10-12 – Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri. 11 Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri? 12 Akasema, Bila shaka mimi nitakuwa pamoja nawe; na dalili ya kuwa nimekutuma ndiyo hii; utakapokuwa

umekwisha kuwatoa hao watu katika Misri, mtamwabudu Mungu katika mlima huu.

2. Mapambano ya Mungu na Farao kupitia Musa , Kut. 7:15-18 – Mwendee Farao asubuhi; tazama, atoka kwenda majini; nawe simama karibu na ufuo wa mto ili upate kuonana naye; na ile fimbo iliyogeuzwa kuwa nyoka utaichukua mkononi mwako. 16 Nawe umwambie, Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nije kwako, kusema, Wape watu wangu ruhusa, ili wapate kunitumikia jangwani; nawe, tazama! Hujasikia hata sasa. 17 Bwana asema, Katika jambo hili utanijua ya kuwa mimi ndimi Bwana; tazama, nitayapiga haya maji yaliyo mtoni kwa fimbo hii niliyo nayo mkononi mwangu, nayo yatageuzwa kuwa damu. 18 Na hao samaki walio mtoni watakufa, na huo mto utatoa uvundo; nao Wamisri watachukizwa kuyanywa maji ya mtoni. 3. Ugumu wa moyo wa Farao unapelekea kwenye hukumu ya Mungu juu ya Misri kupitia miujiza ya kimungu, ishara na maajabu, Kut. 5:1-2 – Hata baadaye, Musa na Haruni wakaenda wakamwambia Farao, wakasema, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Wape watu wangu ruhusa waende, ili kunifanyia sikukuu jangwani. 2 Farao akasema, Bwana ni nani, hata niisikilize sauti yake, na kuwapa Israeli ruhusa waende zao? Mimi simjui Bwana, wala sitawapa Israeli ruhusa waende zao.

4. Mungu kujikombolea watu wake kwa kusudi la ibada na utumishi, Kut. 3:19 – Nami najua ya kuwa huyo mfalme wa Misri hatawapa ruhusa mwende zenu, la, hata kwa mkono wa nguvu.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software