Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa
Kipindi cha 2 : Wito wa Wokovu
25
B. Kanuni kwa watu wa Mungu leo
1. Muhtasari wa kusudi la Mungu la ukombozi
a. Mungu pekee ndiye Muumba na Mwenye Enzi Kuu juu ya ulimwengu wote mzima.
(1) Zab. 92:8 – Bali Wewe, Bwana, U Mtukufu hata milele.
(2) Isa. 54:5 – Kwa sababu Muumba wako ni mume wako; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote.
b. Mungu amedhamiria kuushinda uasi wa shetani (1 Yoh. 4:4).
c. Mungu amekusudia kurejesha na kukomboa uumbaji wake, Rum. 8:19-21 – Kwa maana
viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. 20 Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini; 21 kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu
d. Mungu atauthibitisha upya utawala wake kwa kuwaokoa watu kwa ajili yake mwenyewe, Tit. 2:11-15.
e. Mungu atajumlisha vitu vyote katika Mwanawe, Masihi na Bwana, Efe. 1:9-10 – akiisha kutujulisha siri ya mapenzi yake, sawasawa na uradhi wake, alioukusudia katika yeye huyo. 10 Yaani, kuleta madaraka ya wakati mkamilifu atavijumlisha vitu vyote katika Kristo, vitu vya mbinguni na vitu vya duniani pia. Naam, katika yeye huyo;
Made with FlippingBook Digital Publishing Software