Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

26

Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa

2. Ahadi ya wazi ya wokovu

a. Hadithi ya Utukufu wa Mungu na nafsi ya Yesu wa Nazareti (Lk 4:16-18 rej. Isa. 61:1-4).

b. Injili ya Ufalme, Mk. 1:14-15 – Hata baada ya Yohana kutiwa gerezani, Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya Mungu, 15 akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili.

c. Tubuni dhambi zenu na kuamini Habari Njema.

(1) Mdo 2:38 – Petro akawaambia, “Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.” (2) Mdo. 20:21 – nikiwashuhudia Wayahudi na Wayunani wamtubie Mungu, na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.

3. Mwitikio thabiti wa ufuasi (Lk 14:26-33)

a. Wa haraka, Mt. 4:19-22 – Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu. 20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. 21 Akaendelea mbele, akaona ndugu wengine wawili, Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, ambao walikuwamo chomboni pamoja na Zebedayo baba yao, wakizitengeneza nyavu zao; akawaita. 22 Mara wakakiacha chombo na baba yao, wakamfuata. b. Wa bila masharti, Lk. 9:23-26 – Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate. 24 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi

Made with FlippingBook Digital Publishing Software