Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

30

Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa

na kuyahubiri haya, na kunitengenezea, tangu nilipowaweka watu wa kale? Na mambo yanayokuja na yatakayotokea, wayatangaze.”

2. Watu wamepotea na pasipo ukombozi ambao Mungu pekee hutoa kupitia Yesu Kristo, wataangamia, Yn. 3:16, 36.

3. Mungu anawaita watu wote kila mahali watubu na kumwamini Yesu Kristo, Mdo. 17:30-31 – Basi, zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hazioni; bali sasa anawaagiza watu wote wa kila mahali watubu. 31 Kwa maana ameweka siku atakayowahukumu walimwengu kwa haki, kwa mtu yule aliyemchagua; naye amewapa watu wote uthabiti wa mambo haya kwa kumfufua katika wafu. 4. Wahudumu wa kweli wa mijini, kama Musa, wamekutana na “kijiti kinachowaka moto”; hivyo ni lazima watakuwa wameitikia wito wa Mungu katika toba ya kibinafsi na imani ( huwezi kutoa usichokuwa nacho; huwezi kupoteza kile ambacho hujawahi kuwa nacho ).

5. Wito wa kuokolewa pia ni wito wa ufuasi: mwitikio wa haraka kwa Yesu, usio na masharti, na ubadilishao.

B. Kuhusianisha somo na maisha yako leo

1. Je, ninamtambua BWANA kuwa Muumba wangu na Muumba wa vitu vyote?

2. Je, ninaelewa na kuamini muhtasari wa Biblia wa Hadithi ya utukufu wa Mungu?

3. Je, nimetubu na kumwamini Yesu Kristo kama Masihi na Bwana wa wote?

Made with FlippingBook Digital Publishing Software