Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

Kipindi cha 2 : Wito wa Wokovu

29

Injili ya Tano

Hii naiita injili ya tano. Tuna Injili za Mt. Mathayo, Mt. Marko, Mt. Luka, na Mt. Yohana, na sasa ya tano, Injili ya Watakatifu Waumini wa Kiinjili. Injili hii ya Waumini wa makanisa ya Kiinjili imechukuliwa kutoka katika aya za hapa na pale katika Injili nyingine nne. Mara nyingi huwa tunachukua mstari mmoja hapa, mstari mmoja pale, aya zote zinazotoa jambo fulani tunalolitamani, mistari yote yenye ahadi kama Yohana 3:16 na Yohana 5:24, tukiweka mistari hii yote pamoja ili kuunda theolojia ya utaratibu juu ya wokovu. Halafu tunasahau mistari mingine, matakwa na maagizo ya Yesu Kristo. Hii ni injili ya tano, injili ya ahadi, injili inayomtambulisha Yesu kama Mwokozi binafsi – pekee. Ni nani aliyeturuhusu kumwasilisha Yesu kama hivi au vile na si kama alivyo kiuhalisia? Hebu tufikiri, wanandoa wachanga wanafunga ndoa. Na mchungaji anapomuuliza bwana arusi, “utamchukua mwanamke huyu kuwa mke wako?” kijana huyo anasema, “Mchungaji, ninamkubali msichana huyu kama mpishi wangu binafsi, msafisha vyombo, na kijakazi.” Hivi msichana huyo angesemaje? Angesema, “Subiri kidogo. Nitaenda kupika, ndio. Na nitaenda kuosha vyombo. Nitaenda kusafisha nyumba. Lakini mimi si mjakazi. Nitakuwa mke wako, na lazima pia unipe upendo wako, moyo wako, nyumba yako – kila kitu.» Hiyo ndio ndoa! Ndivyo ilivyo pia kwa Yesu. Ni kweli yeye ni Mwokozi. Kisha tunakuwa wa kiroho na kumkubali kama mponyaji pia. Subiri kidogo. Yeye yuko kama alivyo. Hatuwezi kumkata Yesu vipande vipande na kuchukua kipande tunachokipenda zaidi. Sisi ni kama watoto wanaopewa mkate na jemu. Wanakula jemu na kukurudishia mkate. Kisha unaweka jemu zaidi juu yake na wanalamba jemu tena na kukupa mkate. Hivyo ndivyo tunavyotaka kufanya na Yesu. Tunataka kuchukua jemu na kurudisha mkate. Tunapaswa kula mkate na jemu. Mbingu zinaweza kuwa jemu, lakini Bwana Yesu ndiye Mkate wa Uzima.

~ Juan Carlos Ortiz. Call to Discipleship . Plainfield, NJ: Logos International Press, 1975. uk. 55-56.

II. Kuitikia Wito

A. Matokeo yake kwa huduma ya mjini

1. Mungu ndiye anayetawala, na anafanya kila kitu kwa kusudi lake kuu. Hakuna eneo, mtaa, jamii, jiji, au mkoa unaomtisha , Isa. 44:6-7 – Bwana, Mfalme wa Israeli, Mkombozi wako, Bwana wa majeshi, asema hivi; “Mimi ni wa kwanza, na mimi ni wa mwisho; zaidi yangu mimi hapana Mungu. 7 Naye ni nani kama mimi atakayeita,

Made with FlippingBook Digital Publishing Software