Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

Kipindi cha 3 : Wito wa Utakatifu

37

b. Kusudi la Mungu ni kuusimamisha upya utakatifu wake katika ulimwengu wake wote.

c. Utawala wa ufalme wa Mungu umetofautishwa na kutengwa na mfumo wa ulimwengu wenye choyo, tamaa, na kiburi.

2. Mungu amejikombolea watu wake watakatifu; tumeitwa kuwa watakatifu, 1 Kor. 1:2 – Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, wale waliotakaswa katika Kristo Yesu, walioitwa wawe watakatifu, pamoja na wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo kila mahali, Bwana wao na wetu.

a. Limenunuliwa kama mali maalum ya Mungu mwenyewe (Tit. 2:14).

b. Limetengwa na ulimwengu liwe la Mungu mwenyewe kwa ajili ya mapenzi yake na kusudi lake (Ufu. 4:11; 2 Tim. 1:9).

c. Linakusudiwa kuakisi utakatifu wa utukufu wa Mungu kupitia maisha yake na uwepo wake wa kinabii na kuhubiri kwake, 1 Pet. 2:9-10 – Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; 10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.

3. Watu wa Mungu wanapaswa kukumbatia na kuyathamini mapokeo ya kinabii na kitume ambayo juu yake imani na utendaji wetu umejengwa.

a. 2 The. 2:15 – Basi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ama kwa maneno, ama kwa waraka wetu.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software