Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

36

Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa

huwasilishwa kwa njia ambayo inahusisha matakwa ya Kiungu juu ya mwenendo wa waumini. Hawa wanaitwa hagioi, “watakatifu,” yaani, “waliotakaswa”. Utakatifu huu si ambao mtu anaweza kuufikia kwa kutimiza vigezo fulani vya kidini, ni hali ambamo Mungu katika neema huwaita wanadamu; hata hivyo waamini bado wanaitwa kuendelea kujitakasa (kulingana na wito wao, 2 Tim. 1:9), wakijitakasa wenyewe kutoka kwenye unajisi wote, wakiacha dhambi, wakiishi maisha “matakatifu,” 1 Pet. 1:15; 2 Pet. 3:11, na kuwa na ushirika na Mungu katika utakatifu wake. Kwa hiyo, katika lugha ya picha watakatifu wanatajwa kuwa “hekalu takatifu,” 1 Kor. 3:17 (kanisa la mahali); Efe. 2:21 (Kanisa zima), rej. Efe. 5:27; “ukuhani mtakatifu,” 1 Pet. 2:5; “taifa takatifu,” 1 Pet.2:9. “Ni wazi kwamba hagios na maneno ya jamii yake . . . yanaeleza jambo fulani la zaidi na la juu zaidi kuliko hieros , takatifu, inayohusianishwa na Mungu kwa nje; . . . jambo zaidi ya semnos , inayostahili, yenye heshima; jambo zaidi ya hagnos , safi, isiyo na unajisi. Hagiosis . . . katika namna pana zaidi. . . . Ni tabia ya kumfanania Mungu.”

~ G.B. Stevens, in Hastings’ Bible Dictionary Vine’s Complete Expository Dictionary, Old Testament utafutaji-neno, toleo tepe katika programu ya kompyuta

B. Kanuni kwa watu wa Mungu leo

1. Mungu ameifunua nafsi yake kama mtakatifu na aliyetengwa, 1 Pet. 1:14-19 – Kama watoto wa kutii

msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu; 15 bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; 16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu. 17 Na ikiwa mnamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni. 18 Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu; 19 bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.

a. Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo ni Mungu mtakatifu.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software