Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa
Kipindi cha 6 Wito wa Utumishi Kuelewa Wito Halisi kama Wito wa Utumishi
Kwa nini tuelezee dhana zifuatazo kama wajibu wa wito wa Mungu?
• Zipo katika namna ambayo ingawa zinajumuisha kila mtu ndani ya jumuiya ya kiagano zinafanywa kwa namna maalum, ya kipekee, na ya kibinafsi. • Ni maalum katika namna kwamba ingawa jumuiya imeunganishwa chini ya kusudi moja la agano, hali, vipawa, malezi, na uwezo wa watu binafsi hutofautiana sana kulingana na majaliwa ya Mungu. • Ni maalum katika maana ya kwamba Mungu huongoza hatua za kila mtu na familia katika jumuiya na huita kila mmoja kulingana na mapenzi yake na kusudi lake kuu, kwa ajili ya utukufu wake na manufaa ya jumuiya.
I. Kuelewa Wito Halisi kama Wito wa Utumishi
Mt. 20:25-28 Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha. 26 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu; 27 na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu bali mtu ye yote anayetaka kuwa na awe mtumwa wenu; 28 kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.
Kwa kuzingatia umuhimu wa viongozi wenye uwezo katika Kanisa – na katika ulimwengu wa biashara na serikali, pia – tunaweza kutarajia kwamba Biblia ingetumia neno hilo mara nyingi zaidi. Kimsingi, Biblia ya King James (ambayo wengi wa kizazi changu wamelelewa nayo) inatumia neno kiongozi mara sita pekee. Mara nyingi zaidi, nafasi hiyo inaitwa mtumishi. Hatusomi kuhusu “Musa, kiongozi wangu,” bali “Musa mtumishi wangu.” Na hivi ndivyo Kristo alivyofundisha hasa. Yesu alikuwa mwanamapinduzi, si katika maana ya vita vya msituni, bali katika mafundisho yake juu ya uongozi. Neno mtumishi linazungumza kila mahali juu ya hadhi ya chini na heshima ya chini. Watu wengi hawavutiwi na jukumu la chini kama hilo. Hata hivyo, Yesu alipotumia neno hilo, lilikuwa ni kisawe cha ukuu. Na hilo lilikuwa wazo la kimapinduzi. Kristo alifundisha kwamba Ufalme wa Mungu ni jumuiya ambayo kila mwana-jumuiya anamtumikia mwenzake. Paulo aliandika kwa namna hiyo hiyo: “Tumikianeni kwa upendo” (Gal. 5:13). Huduma yetu ya upendo inapaswa kuenea pia kwa ulimwengu wenye uhitaji unaotuzunguka. Lakini katika makanisa mengi, ni watu wachache ndio hubeba mzigo. Yesu alijua kwamba wazo la kiongozi kuwa “mtumishi mwenye upendo kwa wote” halingewavutia watu wengi. Kujitimizia matakwa yetu binafsi ni dhamira ya kawaida zaidi. Lakini “mtumishi” ndio kigezo chake kwa wale wanaotaka kuongoza katika Ufalme wake.
~ J. Oswald Sanders. Spiritual Leadership . Toleo la 2. Chicago: Moody Press, 1994. uk. 21-22.
69
Made with FlippingBook Digital Publishing Software