https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

1 9 6 /

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

2. Hakuna ruhusa wala mwanya wa uonevu au wizi, Law. 19:13.

F. Fungua mikono, fungua moyo daima kwa maskini : ukarimu mkubwa ulipaswa kutendeka kwa yeyote aliyepatikana kuwa maskini au mhitaji, Kum. 15:7-11.

1. Pasiwe na ugumu wa moyo au chuki juu ya maskini katika nchi.

2. Kinachoshughulikiwa hapa ni msukumo wa ndani: Mfumbulie kwa kweli mkono wako nduguyo, mhitaji wako, maskini wako, katika nchi yako, Kum. 15:11.

G. Rasilimali zilizotengwa kwa ajili ya maskini : sehemu fulani za zaka zilipaswa kutolewa kwa maskini, ambazo zilifungamanishwa moja kwa moja na baraka za Mungu juu ya maisha na mazao yao.

4

1. Zaka na mahitaji yatolewe ili kukidhi mahitaji ya makuhani, pamoja na “mgeni, yatima, na mjane” (yaani, watu walio hatarini zaidi katika jamii ya agano), Kum. 14:28-29.

2. Kuweka kando fadhila kwa ajili ya kuwagawia walio hatarini kulihusishwa moja kwa moja na uhusiano wa mtu na Mungu na jamii yenyewe ya agano, Kum. 26:12-15.

H. Sikukuu na Sherehe, pia : maskini walipaswa kujumuishwa katika karamu na sherehe pamoja na watu wa Mungu.

1. Sikukuu ya Majuma, Kumb. 16:10-12.

2. Sikukuu ya Vibanda, Kumb. 16:13-14.

Made with FlippingBook Annual report maker