Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

maandiko...?” (Mathayo 21:42). Masadukayo walipomwuliza swali, aliwajibu, “Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu” (Mt. 22:29). Yesu mara nyingi alirejelea ulazima wa Maandiko kutimizwa (taz. Mt. 26:54, 56; Yh 13:18; 17:12). Katika Luka 24:44 Yesu alithibitisha kwamba kila kitu kilichoandikwa juu yake mwenyewe katika Maandiko “lazima kitimie” (rej. mst. 45). Mara nyingi, Kristo alitumia neno “Maandiko” katika ujumla wake, bila kutaja kifungu maalum cha Agano la Kale (taz. Yh 7:38, 42; 19:36; 20:9). Kwa hiyo, Alitumia maneno “kama maandiko yasemavyo” kwa namna fulani sawa na usemi wa sasa “kama Biblia isemanavyo.” Yesu aliyachukulia Maandiko kama ufunuo dhahiri wa Mungu kwa mwanadamu. Alisema, “Maandiko hayawezi kutanguka” (Yh 10:35). Hivyo ndivyo Yesu alivyoyachukulia mamlaka ya kimungu ya maandiko ya Agano la Kale—maandiko ambayo yalikuwa kanoni ya imani, ambayo lazima yatimizwe, na ambayo hayangeweza kutanguka. Imeandikwa Kinachohusishwa kwa karibu na neno “Maandiko” ni kirai “imeandikwa.” Yesu mara nyingi alitumia kirai hiki kuthibitisha mamlaka ya kiungu ya mafundisho yake. Kirai hiki kinapatikana mara tisini na mbili katika Agano Jipya. Kwa kawaida kinatumika kurejelea kifungu fulani cha maandiko; wakati mwingine, hata hivyo, kirai hiki kinachukua umuhimu mpana na kuelekeza wasikilizaji kwenye Agano la Kale katika ujumla wake. Kwa mfano, Yesu alisema, “Lakini kwa nini imeandikwa juu ya Mwana wa Adamu [b] ya kwamba itampasa kuteswa na kudhalilishwa?” (Mk 9:12, TKU). Pengine harejelei hapa kifungu maalum cha Agano la Kale bali mada inayopatikana kote katika Agano la Kale (rej. Mwa. 3:15; Zab. 22; Isa. 53). Mahala pengine Yesu alisema, “… kila kitu kilichoandikwa na manabii kumhusu Mwana wa Adamu kitatimizwa” (Luka 18:31, NEN). Hapa ni dhahiri kwamba kirai hiki kinatumika kurejelea ujumla wa mambo

10

Made with FlippingBook Digital Publishing Software