Kristo: Mada Kuu Ya Biblia
yaliyoandikwa. Katika Luka 21:22, alisema, “Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapatilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa .” Kando na marejeo haya ya jumla ya Agano la Kale chini ya kirai “imeandikwa,” kuna nukuu nyingi za watu binafsi ambazo zinadhihirisha kwamba Yesu katika matamko yake alithibitisha mkusanyiko fulani wa maandiko wenye mamlaka, wenye asili ya kimungu, na usioweza kutanguka. Linganisha, kwa mfano, kwamba (1) Yesu alimpinga Shetani kwa nukuu tatu zenye nguvu za Agano la Kale zilizotanguliwa na “ imeandikwa ” (Mt. 4:4, 7, 10). (2) Yesu alilisafisha hekalu kwa mamlaka akisema kwamba “ Imeandikwa , Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala” (Mt. 21:13). (3) Alitamka ole juu ya msaliti wake, kwa msingi wa kwamba “ imeandikwa ” (Mt. 26:24). (4) Yesu alikemea unafiki wa kidini, kwa maneno “kama ilivyoandikwa ” (akinukuu Isa. 29:13 kwenye Marko 7:6). (5) Alithibitisha umasihi wake mwenyewe kwa kutafuta na kusoma “mahali palipoandikwa , Roho wa Bwana yu juu yangu…” (Luka 4:17-18). (6) Yesu alijibu swali la mwanasheria kwa habari ya jinsi ya kuurithi uzima wa milele kwa kusema, “ Imeandikwa nini katika torati?” (Lk 10:26). (7) Aliegemeza mamlaka yake mwenyewe na utambulisho wake pamoja na Mungu kwa msingi wa ukweli kwamba “ imeandikwa katika manabii” (Yh 6:45; taz. 10:34). (8) Yesu hata alithibitisha mamlaka ya kile kilichoandikwa (katika Agano la Kale) licha ya ukweli kwamba viongozi wa kidini wa siku zake walitaka kumwua kwa sababu hiyo hiyo (rej. Lk 20:16-17). Ili Litimie Usemi mwingine uliotumiwa na Yesu kurejelea mamlaka ya Agano la Kale kwa ujumla ni “ili litimie.” Usemi huu unapatikana mara thelathini na tatu katika Agano Jipya. Ingawa kauli hii kwa kawaida inatumiwa kunukuu kifungu fulani cha Agano la Kale, wakati mwingine imetumiwa kwa njia ya jumla zaidi ikirejelea Agano la Kale kwa ujumla. Mfano mzuri wa matumizi ya jumla ya kauli hii unatoka katika Hotuba ya Mlimani
11
Made with FlippingBook Digital Publishing Software