Kristo: Mada Kuu Ya Biblia
(Mt. 5:17), ambapo Yesu alisema, “ Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza .” Baada ya kufufuka kwake, Kristo alitoa uthibitisho sawa na huo kwamba yote yaliyoandikwa kumhusu Yeye katika Torati, Manabii, na Zaburi “ lazima yatimie ” (Luka 24:44). Katika Luka 21:22 Yesu anatazamia wakati ujao ambapo “yote yaliyoandikwa” yatatimizwa . Katika injili ya Mathayo pekee usemi huu umetumika mara kumi na tano. Yesu alisema alibatizwa ili kutimiza haki yote (Mt. 3:15); Alikuja katika ulimwengu huu ili kutimiliza Torati na Manabii, na ni lazima afe, vinginevyo “ Yatatimizwaje basi maandiko, ya kwamba hivyo ndivyo vilivyopasa kujiri?” (Mathayo 26:54). Torati Neno Torati [Sheria] kwa kawaida linatumika kimahususi kumaanisha vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale, vyenye Torati ya Musa (rej. Lk 2:22; Yh 1:45). Wakati mwingine, hata hivyo, linarejelea Agano la Kale kwa ujumla wake. Katika Mathayo 5:18, kwa mfano, Yesu alisema, “Kwa maana, amin, nawaambia, Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka, yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka, hata yote yatimie.” Hapa sio tu kwamba Yesu anatangaza wazi mamlaka ya mwisho ya Torati bali anaihusianisha kwa uwazi “Torati” na “Torati na manabii” (mst. 17), yaani, Maandiko yote ya Agano la Kale yanarejelewa kwa ujumla kama Torati. Kuna vifungu vingine ambamo Kristo anathibitisha mamlaka ya kiungu ya Agano la Kale kama Sheria ya Mungu kwa ujumla. Katika Yohana 10:34, kwa mfano, Yesu aliwaambia Wayahudi, “Je! Haikuandikwa katika torati yenu…?” baada ya kuwapa nukuu ya Zaburi 82:6. Hapa neno Torati linajumuisha kitabu cha Zaburi. Mahali pengine, kuna marejeo kama hayo ambapo Yesu anatumia maneno kama “torati yao” (yaani ya Wayahudi, Yh 15:25). Vivyo hivyo, watu wengine katika nyakati za Agano Jipya walilirejelea Agano la Kale kama Sheria ya Wayahudi (rej. Mdo 25:8; Yh 18:31; Yh 12:34).
12
Made with FlippingBook Digital Publishing Software