Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

Torati na Manabii Moja ya majina ya kawaida ya Agano la Kale lilikuwa “Torati na Manabii.” Kirai hiki kinapatikana takriban mara kumi na mbili katika Agano Jipya. Yesu alizungumzia “Torati na Manabii” (1) kama kielelezo cha maadili ya kweli (Mt. 7:12), (2) ili kuonyesha dira nzima ya kanoni ya Maandiko ya Agano la Kale (Mt. 11:13), (3) kama yale ambayo alikuja kuyatimiza (Mt. 5:17). Neno la Mungu Kirai kingine kinachoakisi mamlaka kamili ya Maandiko ya Agano la Kale ni “Neno la Mungu.” Agano Jipya linatumia jina hili mara kadhaa likirejelea Agano la Kale kwa jumla wake. Katika Warumi 9:6, kwa mfano, Paulo anasema, “Si kana kwamba neno la Mungu limetanguka”; Waebrania 4:12 inathibitisha kwamba “ neno la Mungu li hai na lina nguvu” (taz. pia 2 Kor. 4:2; Ufu. 1:2). Katika Yohana 10:35, Yesu, akitumia kirai “ neno la Mungu ” sambamba na neno “maandiko,” alithibitisha kwamba “haliwezi kutanguka.” Marko 7:13 inaweka msisitizo zaidi, maana hapa Yesu anaweka tofauti ya wazi kati ya “mapokeo” ya Wayahudi na “neno la Mungu.” Yesu aliwashutumu akisema, “Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu” (Mt. 15:6). Uchunguzi huu hapo juu unatoa uthibitisho pasina shaka kwamba Yesu wa Injili alithibitisha tena na tena, kama mojawapo ya mikazo mikuu ya huduma Yake, kwamba maandiko matakatifu ya Agano la Kale la Kiyahudi, yaliyotajwa kama “Maandiko,” “Torati”, na “Torati na Manabii,” yalikuwa ni “Neno la Mungu” lisiloweza kutanguka, lisiloharibika na lisilopingika. Kristo ndiye ufunguo wa uvuvio wa Agano la Kale kwa sababu bila shaka alilithibitisha; mtu hawezi kushambulia mamlaka ya Agano la Kale bila kupinga uadilifu wa Kristo.

13

Made with FlippingBook Digital Publishing Software