Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

Ahadi ya Kristo Kuhusu Uvuvio wa Agano Jipya Mamlaka ya kiungu ambayo Yesu aliyathibitisha kuhusu Agano la Kale aliyaahidi pia kwa habari ya Agano Jipya. Mara kadha wa kadha Yesu aliwaahidi wanafunzi wake kwamba baada ya kuondoka kwake (kupaa), Roho Mtakatifu angewaongoza katika yale ambayo wangeyazungumza juu yake. Maandiko ya Agano Jipya ni utimilifu wa ahadi hizi. Ni katika mantiki hii Kristo pia ni ufunguo wa uvuvio wa Agano Jipya. Ahadi ya Kristo kwa Wanafunzi Maisha ya Yesu yaliyojaa shughuli nyingi na utume wake wa kiungu havikumpatia nafasi ya kuweka mafundisho yake katika maandishi. Kazi hii aliwaachia wanafunzi wake kwa ahadi kwamba Roho Mtakatifu “atawakumbusha” mambo yote kuhusu Kristo na “kuwaongoza katika kweli yote.” Yesu aliahidi tena na tena mwongozo kuhusiana na yale ambayo wanafunzi walifundisha. Hata wale kumi na wawili walipopewa jukumu la kuhubiri habari za “ufalme wa mbinguni” kwa mara ya kwanza (Mt. 10:7), Yesu aliwaahidi, akisema, “Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema. Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.” (mst. 19 20; taz. Lk 12:11-12). Ahadi hiyo hiyo ya msingi pia ilitolewa kwa wale sabini walipopewa mamlaka ya kuhubiri habari za “ufalme wa Mungu” (Lk 10:9). Yesu alisema, “Awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi” (Lk 10:16). Baadaye, kwenye Mlima wa Mizeituni, Yesu aliwaahidi tena wanafunzi wake hivi: “…msitafakari kwanza mtakayosema, lakini lo lote mtakalopewa saa ile, lisemeni” (Mk 13:11).

14

Made with FlippingBook Digital Publishing Software