Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

Tena baadaye, kwenye Karamu ya Mwisho, Yesu alifafanua ahadi yake kwa wanafunzi kumi na mmoja kwa uwazi zaidi, akisema, “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote , na kuwakumbusha yote niliyowaambia .” (Yh 14:26). Pia aliwaambia, “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote ” (Yh 16:13). Agizo Kuu la Kristo, lililotolewa baada ya kufufuka kwake, lina ahadi ile ile: “Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu” ili “kwamba mataifa yote watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi” (Lk 24:49, 47). Katika Mathayo 28:18-19, Yesu anawaagiza wanafunzi kwa “mamlaka yote mbinguni na duniani” kwenda “kufanya mataifa yote kuwa wanafunzi . . . na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi,” akiwaahidi uwepo wake pamoja nao daima katika utekelezaji wa agizo hilo la kufundisha juu yake ( mst . 20). Wanafunzi Wapokea Ahadi ya Kristo Ahadi ya Kristo ya kuwaelekeza wanafunzi katika yale yote ambayo waliyafundisha juu yake ndiyo ufunguo wa mamlaka ya kimungu ya Agano Jipya, na madai ya wanafunzi kuhusu mamlaka hayo ni utimilifu wa ahadi hiyo. Kwa ufupi, 1. Chochote ambacho mitume wa Yesu walifundisha kilitoka kwa Roho Mtakatifu. 2. Agano Jipya ni yale ambayo mitume walifundisha. 3. Kwa hiyo, Agano Jipya lilitokana na Roho Mtakatifu. Ni jambo lililo dhahiri sana kwamba mitume na washirika wao walipokea ahadi ya Kristo katika mafundisho ya maandiko yao yaliyoongozwa na Roho Mtakatifu.

15

Made with FlippingBook Digital Publishing Software