Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

Madai ya Kuendeleza Mafundisho ya Kristo Injili ya Luka, kwa mfano, inadai kutoa maelezo sahihi ya yote ambayo “Yesu alianza kufanya na kufundisha” (Mdo 1:1; taz. Lk 1:3-4). Kwa hiyo, kitabu cha Matendo kinatoa kumbukumbu ya yale ambayo Yesu aliendelea kufundisha kupitia wanafunzi wake. Linganisha dai hili na ukweli kwamba kanisa la kwanza lina sifa ya kudumu “katika fundisho la mitume ” (Mdo 2:42), mamlaka ya mwisho ya matamko yao (rej. Mdo 15:22), na kule kuwaombea watu hata kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu kupitia huduma yao (rej. Mdo 8:14-17; 10:45; 19:6). Kulinganisha Maandiko Yao na Maandiko ya Agano la Kale Ni dhahiri zaidi kwamba waandishi wa Agano Jipya walidai kutimizwa kwa ahadi ya Kristo kwa kuweka maandiko yao kwenye kiwango sawa na Maandiko ya Agano la Kale. Hayo ndiyo madai yaliyotolewa katika Waebrania 1:1-2, ambayo inatangaza kwamba Mungu ambaye zamani za kale alinena kwa njia ya manabii, katika siku hizi za mwisho amesema nasi kupitia Mwanawe, ujumbe ambao “…kwanza ulinenwa na Bwana, kisha ukathibitika kwetu na wale waliosikia [yaani, mitume]” (Ebr. 2:3). Petro, katika waraka wake wa pili (3:15-16), anaziweka nyaraka za Paulo kwenye fungu moja na “ maandiko mengine ,” na 1 Timotheo 5:18 inarejelea injili ya Luka (10:7) kwa kutumia jina “maandiko.” Kauli Ndani ya Vitabu vya Agano Jipya Zinazoonyesha kuwa Vinamamlaka ya Kimungu Uthibitisho mmoja zaidi kwamba waandishi wa Agano Jipya waliyachukulia maandiko yao kuwa utimilifu wa ahadi ya Kristo unatokana na madai yaliyomo ndani ya vitabu vyao. Kila kitabu kwa namna yake, moja kwa moja au kwa namna isiyo ya moja kwa moja, kinadai kuwa kimeandikwa kwa mamlaka ya kimungu.

16

Made with FlippingBook Digital Publishing Software