Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

Injili, kwa mfano, zinajipambanua kama maelezo yenye mamlaka ya utimilifu wa unabii wa Agano la Kale katika maisha ya Kristo (rej. Mt. 1:22; 2:15, 17, 23; 4:14, nk.). Luka alimwandikia Theofilo ili kwamba apate “kujua hakika,” yaani ukweli kuhusu Kristo (1:1, 4). Yohana aliandika ili kwamba wanadamu wapate “kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo...” (20:31), na anaongeza kusema kwamba “ushuhuda wake ni kweli” (21:24). Kitabu cha Matendo, kwa namna isiyo ya moja kwa moja, kinajifafanua kama kumbukumbu inayoendelea ya yale ambayo Yesu alikuwa ameanza kufanya na kufundisha katika Injili (1:1). Nyaraka za Paulo kila moja ilihusisha madai ya kuwa na mamlaka ya kiungu (rej. Rum. 1:3-5; 1 Kor. 14:37; 2 Kor. 1:1-2; Gal. 1:1, 12; Efe. 3:3; Flp. 4:9; 1:1; 1 Tim. 4:11; 2 Tim. 1:13; 4:1; Tit 2:15; Flm 8). Nyaraka za Jumla pia zinadai kuwa na mamlaka ya kimungu (taz. Ebr. 1:1; 2:3; Yak 1:1; 2 Pet 1:1; 2 Pet 3:2; 1 Yoh 1:1; 2 Yoh 5, 7; 3 Yoh 9, 12; Yud 3; Ufu. 22:9, 18-19). Kanisa la Kwanza Lilithibitisha Dai Hili Yesu aliahidi uvuvio, waandishi wa Agano Jipya walitimiziwa ahadi hii, na Kanisa la Kwanza liliithibitisha. Uthibitisho huo ulidhihirika katika ukweli kwamba vitabu vya Agano Jipya: 1. Vilikukubalika kama maandiko yenye mamlaka (2 The. 2:15); 2. Vilisomwa katika makanisa (1 The. 5:27); 3. Vilisambazwa katika makanisa; 4. Vilinukuliwa na waandishi wengine wa Agano Jipya (rej. 2 Pet 3:2-3 na Yud 17-18; 1 Tim. 5:18 na Luka 10:7); na

17

Made with FlippingBook Digital Publishing Software