Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

5. Vilikusanywa pamoja na maandiko ya Agano la Kale (2 Pet 3:15). Hivyo basi, Kristo ndiye ufunguo wa uvuvio wa Biblia. Alichodai kuhusu asili na mamlaka kamili ya kimungu ya Agano la Kale, alikiahidi pia kwa habari ya maandiko ya mitume katika Agano Jipya. Uthibitisho wa kwamba hilo ni kweli unaonekana katika uhakika wa kwamba uvuvio ambao Kristo aliuahidi, waandishi wa Agano Jipya waliupokea, na Kanisa la Kwanza liliuthibitisha, yaani, kwamba maandiko ya Agano Jipya yalizingatiwa kuwa na mamlaka ya kimungu sawa na maandiko ya Agano la Kale. KRISTO: UFUNGUO WA KANONI YA BIBLIA Neno kanoni kama linavyotumika kuhusiana na Biblia linamaanisha maandiko ambayo yanachukuliwa kuwa “kanuni” (Kiyunani, Kanon ) au “kaida” ya imani na utendaji. Kwa maana hiyo, “kanoni” ya Maandiko ni vile vitabu ambavyo vimeundwa kwa mamlaka ya kimungu. Kwa maneno mengine, kitabu chenye sifa ya “kikanoni” ni kile ambacho kimevuviwa na Mungu. Sifa ya “kikanoni” au mamlaka ya kimungu ya kitabu yalitolewa au kuamuliwa na Mungu, ambaye alikipa mamlaka hayo. Uhalali wa kikanoni, hata hivyo, ulipaswa kubainishwa au kutambuliwa na watu wa Mungu, ambao waliyakubali na kuyakusanya maandiko hayo. Hili linaibua swali kuhusu vigezo au sifa bainifu za kitabu cha kikanoni. Kanisa lingewezaje kutambua vitabu ambavyo Mungu alikuwa amevivuvia? Kanisa la kwanza mara nyingi lilizingatia vigezo kama vile: 1. Je, kitabu hiki kiliandikwa na mtu wa Mungu? 2. Je, mwandishi alithibitishwa kuwa nabii wa Mungu?

18

Made with FlippingBook Digital Publishing Software