Kristo: Mada Kuu Ya Biblia
3. Je, kinaeleza ukweli kuhusu Mungu (kama anavyojulikana kutokana na mafunuo yaliyotangulia)? 4. Je, kina uwezo wa Mungu (k.m., kujenga)? 5. Je, kilikubaliwa na watu wa Mungu? Kwenye orodha hii kunaweza kuongezwa vigezo vingine vinayoingiliana na baadhi ya hivi (hususan kuhusiana na vitabu vya Agano la Kale), kama: Je, kilithibitishwa na Mwana wa Mungu? Je, Yesu alirejelea au kunukuu kitabu hiki kama kitabu cha kikanoni? Ikiwa ndivyo, basi ufunguo wa uthibitisho wa sifa ya kikanoni unaweza kupatikana katika uthibitisho wa Kristo. Tayari tumejifunza juu ya kile ambacho Yesu alifundisha kuhusu mamlaka ya kimungu ya Agano la Kale kwa ujumla. Iwapo inaweza kubainishwa ni vitabu vipi vilivyounda kanoni ya Agano la Kale ambayo Yesu aliirejelea, basi inaweza pia kuthibitishwa ni nini kilichounda kanoni ambayo Yeye aliidhinisha. Kuna mistari kadhaa yenye ushahidi wa kuthibitisha kwamba kanoni ya Kristo ni sawa na ile ya Agano la Kale la Kiyahudi na la Kiprotestanti la nyakati zetu. Agano la Kale la Kiyahudi la leo lina vitabu ishirini na vinne lakini linafanana na Agano la Kale la Kiprotestanti ambalo lina jumla ya vitabu thelathini na tisa kwa sababu lile la Kiyahudi “linaunganisha” Manabii Wadogo kumi na wawili kuwa kitabu kimoja, kadhalika vitabu vya Wafalme na Samweli [kitabu kimoja], Mambo ya Nyakati [kitabu kimoja] na Ezra-Nehemia [kitabu kimoja]. Wayahudi pia wakati fulani waliorodhesha vitabu vyao kuwa ishirini na viwili, kutokana na Ruthu kuunganishwa na Waamuzi, na Maombolezo na Yeremia, hivyo kuendana na idadi ya herufi katika alfabeti ya Kiebrania. Agano la Kale la Kikatoliki, kwa upande mwingine, lina vitabu vingine saba zaidi (na sehemu nne za vitabu), na kufanya jumla ya vitabu arobaini na sita na sehemu
19
Made with FlippingBook Digital Publishing Software