Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

nne za vitabu. Vitabu hivyo vinajulikana kama vitabu vya Apokrifa na vinajumuisha (1) Tobiti; (2) Yudith; (3) Hekima ya Sulemani; (4) Sira; (5) Baruku na Barua ya Yeremia; (6) 1 Wamakabayo; (7) 2 Wamakabayo; (8) Nyongeza ya Esta (10:4-16:24); 11 (9) Sala ya Azaria na Wimbo wa Vijana Watatu (ulioingizwa baada ya Dan. 3:23); (10) Susana (Dan. 13); na (11) Beli na Joka (Dan. 14). Je, Yesu aliviona vitabu hivyo kuwa sehemu ya orodha ya Maandiko yaliyovuviwa? Ushahidi ulio wazi uko kinyume na maoni ya namna hiyo kwa sababu kadhaa. Hata madhehebu ya Kimasihi huko Qumran yalikuwa na vitabu vya Apokrifa lakini ni dhahiri kwamba hayakuvichukulia kuwa na thamani sawa na Maandiko matakatifu. (Milflar Burrows akizungumzia Apokrifa anasema, “Hakuna sababu ya kufikiri kwamba mojawapo ya kazi hizi ziliheshimiwa kama Maandiko Matakatifu” ( More Light on the Dead Sea Scrolls . New York: Viking, 1958, uk. 178). Wasomi wanataja sababu kadhaa tofauti zenye ushahidi unaoonyesha kwamba vitabu vya Apokrifa havikuchukuliwa kama vitabu vya kikanoni huko Qumran: (1) kutokuwepo kwa ufafanuzi wowote juu ya vitabu vya Apokrifa, (2) kushindwa kupata vitabu vyovyote vya Apokrifa vilivyoandikwa kwenye vifaa vya kuandikia vyenye thamani zaidi kama vile ngozi, (3) na hata kutopata vitabu vyovyote vya Apokrifa vilivyoandikwa katika hati zenye herufi maalum (ndefu zaidi), kama ilivyokuwa kwa vitabu vya kikanoni. 2 Ushuhuda wa Yesu Kuhusu Kanoni Kama ilivyokwisha bainishwa, majina ya kawaida zaidi ya kanoni kamili ya Agano la Kale katika siku za Yesu yaliwakilishwa na kirai “Torati na Manabii.” Kirai hiki kinapatikana takribani mara kumi na mbili 1 Katika Agano la Kale la Kiyahudi na la Kiprotestanti, kitabu cha Esta kinaishia na Esta 10:3, na Danieli kinaishia na Dan. 12. 2 Kwa ufafanuzi zaidi wa kipengele hiki ona N. L. Geisler na William Nix, A General Introduction to the Bible (Chicago: Moody, 1988), sura ya 11 au From God to Us , sura ya 8.

20

Made with FlippingBook Digital Publishing Software