Kristo: Mada Kuu Ya Biblia
katika Agano Jipya (taz. Mt. 5:17; Lk. 16:16; Mdo. 24:14), na kila wakati kinakusudiwa kujumuisha Agano la Kale lote (vitabu vyote ishirini na viwili vya Wayahudi au vitabu thelathini na tisa vya Waprotestanti). Katika Mathayo 11:13, upeo wa kirai hiki umeonyeshwa wazi; “Torati na Manabii” inajumuisha maandiko yote yaliyovuviwa tangu Musa hadi Yohana Mbatizaji. Hili bila shaka halifafanui kwa usahihi yaliyomo katika kanoni ya Agano la Kale (hili lazima lithibitishwe kutokana na vyanzo vingine); linachofanya, hata hivyo, ni kubainisha mipaka ya kanoni ya Agano la Kale kama “Torati na Manabii” ya Wayahudi. Kwa hiyo, Agano la Kale lote lilirejelewa katika makundi mawili , Torati na Manabii. 33 Yesu aliziita sehemu hizi mbili “maandiko yote” (Lk 24:27). Kuna ushahidi kutoka kwa jumuiya ya Bahari ya Chumvi huko Qumran kwamba Waesene wakati wa Kristo pia walilirejelea Agano la Kale lote kama Torati na Manabii (Lk 24:27), kama alivyofanya mwandishi wa 2 Wamakabayo (taz. 15:9). Hata hivyo, kulikuwa na mwelekeo wa awali, hata kabla ya siku za Yesu (taz. Dibaji ya Sira, 132 K.K.), wa kuwagawanya Manabii katika sehemu mbili na kupelekea mgawanyo wa sehemu tatu, ambao leo unaitwa Torati, Manabii na Maandiko . Yesu mwenyewe anataja mgawanyo wenye sehemu tatu (Luka 24:44), akiliita Agano la Kale, “Torati ya Musa, na manabii, na zaburi.” Bila kujalisha aina ya mgawanyo, maudhui yalikuwa ni yale yale, kama tutakavyoona hivi punde. Yaliyomo katika Kanoni ya Yesu ya Agano la Kale Josephus, mwanahistoria wa Kiyahudi wa wakati wa Kristo (37-100 B.K), ndiye chanzo bora zaidi kisicho cha kibiblia kuhusiana na yaliyomo katika kanoni ambayo Kristo aliirejelea. Je, kanoni hiyo ilijumuisha vitabu vya Apokrifa au vitabu ishirini na viwili pekee vya Biblia ya Kiebrania ya leo? Jibu la Josephus liko wazi sana:
3 Taz. Manual of Discipline , I, 3; VIII, 15.
21
Made with FlippingBook Digital Publishing Software