Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

Maana hatuna wingi wa vitabu miongoni mwetu. . . lakini vitabu ishirini na viwili tu. . . ambavyo vinaaminika kwa haki kuwa ni vya kimungu; na vitano miongoni mwavyo ni vya Musa. . . [2] manabii waliokuja baada ya Musa waliandika yale yaliyofanyika enzi zao katika vitabu kumi na vitatu. [3] Vitabu vinne vilivyosalia vina nyimbo za Mungu, na kanuni kwa ajili ya mwenendo wa maisha ya mwanadamu. (Josephus, Against Apion I, 8). Ushuhuda wa Josephus unatuelimisha kwa sababu, kwa uwazi kabisa, yeye hajumuishi vitabu vyovyote vilivyoandikwa kati ya mwaka 400 K.K. na 100 B.K (enzi yake). Anasema, Ni kweli historia yetu imeandikwa hasa hasa tangu Artashasta [424 K.K.], lakini haijahesabiwa kuwa na mamlaka kama ile iliyoandikwa zamani na wazee wetu, kwa sababu hapakuwa na mfululizo kamili wa manabii tangu wakati huo. ( ibid. ) Yaani, baada ya Malaki, Wayahudi hawakuona kitabu kingine chochote kuwa kimevuviwa. Sasa, kwa kuwa vitabu vya Apokrifa (vilivyoongezwa rasmi kwenye Biblia mwaka 1546 B.K na Kanisa Katoliki la Roma) viliandikwa katika kipindi cha kati ya miaka ya 200 K.K. na 100 B.K, vingekataliwa waziwazi, kwani kwa hakika haviko kwenye orodha ya vitabu ishirini na viwili ambayo Josephus aliitoa. Matumizi ya Yesu ya Agano la Kale yanasuluhisha swali kuhusu yaliyomo katika kanoni bila kuhitaji uthibitisho wowote kutoka kwa vyanzo vya Kiyahudi vya wakati huo. Kwanza, katika Mathayo 23:35 Yesu alifafanua mipaka ya historia iliyovuviwa ya Agano la Kale kuwa ni kati ya mfia imani Habili ​(Mwanzo) na Zekaria (2 Nya. 24:20 au 36:15-16). Hivyo basi, kwa kuwa kulikuwa na wafia imani wengi wa Kiyahudi katika vitabu vya Apokrifa baada ya wakati huo (taz. 2 Wamakabayo 2, 5, 6, 7), ni dhahiri kwamba maelezo ya Yesu hayawahusu hawa kama sehemu ya historia ya Agano la Kale iliyovuviwa. Zaidi ya hayo, katika nukuu na marejeo mengi kutoka katika kila sehemu kuu ya Agano la Kale tangu sura ya kwanza ya

22

Made with FlippingBook Digital Publishing Software