Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

SURA YA 1 | KRISTO NDIYE UFUNGUO WA BIBLIA

KRISTO: UFUNGUO WA UVUVIO WA BIBLIA Suala la uvuvio wa Biblia linagusa moja kwa moja mamlaka na uadilifu wa Kristo. Ikiwa Biblia si Neno lenyewe la Mungu, la mwisho na lisiloweza kutanguka, kama Yesu alivyodai, basi mtu hawezi kuweka tumaini katika mojawapo ya mafundisho makuu ya kitheolojia ya Kristo, kwa maana hakuna shaka kwamba msisitizo mmojawapo mkuu wa huduma ya Kristo wa Injili ya Agano Jipya ulikuwa ni uthibitisho wa hakika wa mamlaka ya kimungu ya Agano la Kale. Na kile Yesu alichodai kwa habari ya Agano la Kale, alikiahidi kuhusiana na Agano Jipya. Madai ya Kristo Kuhusu Uvuvio wa Agano la Kale Katika siku za Yesu kulikuwa na njia kadhaa za kurejelea Agano la Kale, na nyingi kati ya hizo zilitumiwa na Yesu katika kuthibitisha uvuvio wa kimungu wa maandiko haya matakatifu. Maandiko Pengine njia ya kawaida ya kurejelea Agano la Kale ilikuwa ni kuyaita “Maandiko.” Neno hili limetumika mara hamsini katika Agano Jipya na linachukua maana ya kiufundi. Katika 2 Timotheo 3:16, tunasoma, “Kila andiko lenye pumzi ya Mungu,” na sehemu nyingine za Agano Jipya zinakubaliana na ufafanuzi huu. Maandiko yanaitwa “matakatifu” (2 Tim. 3:15), na kutambuliwa kama kanoni ya kimungu kwa ajili ya imani na matendo ya mwanadamu (Rum. 15:4; 2 Tim. 3:16-17). Katika suala hili la mwisho, kuna mambo muhimu ya kujifunza katika matumizi ya Yesu ya Maandiko. Aliwapinga viongozi wa kidini (Mafarisayo) wa nyakati zake, akiuliza, “Hamkupata kusoma katika

9

Made with FlippingBook Digital Publishing Software