Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

2 Wathesalonike: Kutukuzwa katika Kristo Wakati matazamio ya Kristo yatakapokuwa yametimizwa wakati wa kuja kwake, basi, Paulo anawaambia Wathesalonike, “jina la Bwana wetu Yesu litukuzwe ndani yenu, nanyi [mtukuzwe] ndani yake” (1:12). Watakatifu watatukuzwa ndani yake “atakapokuja ili kutukuzwa katika watakatifu wake” (1:10). 1 Timotheo: Uaminifu katika Kristo Timotheo anakumbushwa juu ya “imani na pendo lililo katika Kristo Yesu” (1:14) na kuendelea kushika “imani na dhamiri njema” (1:19). Paulo alisema alimshukuru Mungu, “kwa sababu aliniona kuwa mwaminifu, akaniweka katika utumishi wake” (1:12). Timotheo alihimizwa: “Piga vita vile vizuri vya Imani” (6:12) na kuishika “siri ya imani” (3:9). Zilikuwa nyakati za uasi (4:1-), ambazo zilidai uaminifu kwa watumishi wa Kristo (rej. 3:11). 2 Timotheo: Usahihi (au uzima) katika Kristo Katika Timotheo wa Pili anahimizwa kudumisha utimamu katika Kristo. “Shika kielelezo cha maneno yenye uzima uliyoyasikia kwangu, katika imani na upendo ulio katika Kristo Yesu” (1:13). “Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima” (4:3). Tito: Uthabiti katika Kristo Kama Timotheo, Tito anahimizwa “kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima ” (1:9, taz. 2:1) na kuwa “ wazima katika imani” (2:2), kadhalika anaambiwa: “Nena maneno hayo... kwa mamlaka yote” (2:15), au, kwa maneno mengine, lazima alishike “neno la hakika” (1:9); lazima awe thabiti katika imani.

121

Made with FlippingBook Digital Publishing Software