Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

Sura hii ilianza na hoja ya kwamba Kristo ndiye mada ya msingi ya kila kitabu katika Biblia. Sasa kwa kuwa jaribio limefanyika la kuhusianisha kila kitabu na Kristo, inapaswa kuonyeshwa tena kwamba licha ya ukweli ulio wazi kwamba kuna mada zingine nyingi zinazoingiliana na mada ya Kristo katika kitabu fulani, na wakati mwingine inawezekana mada nyingine tofauti na ile ya Kristo ikatawala kitabu fulani, hata hivyo ujumbe wa jumla wa Biblia haupati umoja wake kutokana na nyuzi hizi (yaani mada) nyingine za kweli ya Biblia. Badala yake, ni kwa sababu tu nyuzi hizi za kweli ya Biblia zimefumwa katika muundo wa jumla wa kweli ya kibiblia kuhusu Kristo ndiposa zinafunua maana yake kuu. Mada kuu ya Maandiko ni Kristo, na kwa sababu hiyo, kinachobeba umuhimu wa kitabu fulani katika uhusiano wake na kanoni ya Maandiko katika umoja wake si jambo lingine isipokuwa ukweli tu kwamba kweli ya kitabu husika inahusiana na Kristo.

126

Made with FlippingBook Digital Publishing Software