Kristo: Mada Kuu Ya Biblia
havikunukuliwa na Yesu, lakini Samweli na Wafalme vilinukuliwa. Tendo la Dauli kula “mkate wa wonyesho” (1 Sam. 21:1-6) linatajwa katika Mathayo 12:3-4. Huduma ya Eliya kwa mjane (1 Fal 17) imetajwa katika Luka 4:25. Andiko la Mambo ya Nyakati linarejelewa katika Mathayo 23:35 (taz. 2 Nya. 24:21). Huenda ni Ezra-Nehemia vinavyotajwa katika Yohana 6:31 (taz. Neh. 9:15), “Aliwapa chakula cha mbinguni ili wale” (ingawa nukuu hii inaweza kuwa ilichukuliwa kutoka Zab. 78:24 au 105:40). Vitabu vya Esta na Ayubu havirejelewi na Yesu moja kwa moja. Hata hivyo, Zaburi ni mojawapo ya vitabu vilivyonukuliwa mara nyingi na Yesu. Alinukuu kutoka Zaburi (1) akiwa na umri wa miaka kumi na miwili (Lk 2:49, taz. Zab. 26:8; 27:4); (2) katika Hotuba ya Mlimani (Mt. 5:35; 7:23, taz. Zab. 48:2; 6:8); (3) alipokuwa akifundisha makutano (Mt. 13:35, taz. Zab. 78:2); (4) alipoililia Yerusalemu (Mt. 23:37, taz. Zab. 91:4); (5) alipolitakasa hekalu (Mt. 21:16, taz. Zab. 8:2); (6) katika kuwajibu Wayahudi (Mt. 21:42, taz. Zab. 118:22-23); (7) wakati wa Karamu ya Mwisho (Mt. 26:30, taz. Zab. 95-98); (8) msalabani (Mt. 27:46, taz. Zab. 22:1); na (9) baada ya kufufuka kwake (Lk 24:44). Kuna uwezekano kwamba Yesu alirejea Mithali mara moja (25:6-7, taz. Lk 14:8-10) lakini hakurejea waziwazi Mhubiri wala Wimbo Ulio Bora. Yesu alitoa nukuu nyingi kutoka katika kitabu cha Isaya (taz. Lk 4:18 ling. na Isa. 61:1; Yh 12:38 ling. na Isa. 53:1). Yeremia sura ya 18 na 19 zimenukuliwa (kupitia Zek. 11:12-13) katika Mathayo 27:9, na Maombolezo (3:30) inarejelewa katika Mathayo 27:30. Ezekieli hakurejelewa waziwazi na Yesu, lakini kurejelea kwake “maji yaliyo hai” katika Yohana 7:38 kunaweza kuwa dokezo la Ezekieli 47:1. Danieli anatajwa waziwazi na Kristo katika Mathayo 24:15 (taz. Dan. 9:27), aliporejelea “chukizo la uharibifu.” Wale Kumi na Wawili (Manabii Wadogo) wamenukuliwa mara kadhaa (taz. Hos 10:8 ling. na Lk 23:30; Zek. 13:7 ling. na Mt. 26:31; Mal. 4:5 ling. na Mt. 17:11). Yesu alinukuu
24
Made with FlippingBook Digital Publishing Software