Kristo: Mada Kuu Ya Biblia

Yoshua na waandamizi wake waliiona Torati ya Musa kuwa takatifu na yenye mamlaka ya kimungu: (1) Yoshua , mwanzoni mwa huduma yake, aliamuru Torati ya Musa kwa watu (Yos. 1:7-8), na kuwahimiza mwishoni mwa siku za uhai wake “kuyashika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha torati ya Musa” (23:6); (2) Katika Waamuzi Torati ya Musa inaendelea kutambuliwa (3:4) na vilevile katika Ruthu (rej. 4:1-12); (3) Wakati wa 1 na 2 Samweli , Torati ya Musa inarejelewa kama Sheria ya BWANA na ya Musa (1 Nya. 16:40; 22:12); (4) Katika 1 na 2 Wafalme Torati ya Musa inaendelea kutambuliwa (1 Falm 2:3; 2 Falm 18:6); (5) Wakati wa utumwa wa Babeli Yeremia (8:8; 15:1) na Danieli (9:11) wanarejelea Torati ya Musa, na (6) baada ya uhamisho mfumo wa Walawi uliwekwa upya “kama vilivyoandikwa katika chuo cha Musa” (Ezra 6:18), na makuhani wa siku za Nehemia , “walisoma katika kitabu cha Musa masikioni mwa watu” (Neh. 13:1). Hatimaye, Malaki , nabii wa mwisho wa Agano la Kale, aliwaonya watu “kuikumbuka sheria ya mtumishi wangu Musa” (4:4). Kutokana na hili, mtu angehitimisha kwamba katika Agano la Kale vitabu vya Musa vilitambuliwa na watu wa Mungu, vikawekwa katika fungu la peke yake, na kuhifadhiwa kama Neno “takatifu” la Mungu. Manabii baada ya Musa Vitabu vya Musa viliwekwa katika fungu la peke yake kwa sababu alikuwa mwandishi wa vitabu vyote hivyo na mtoa sheria mkuu wa Israeli. Lakini baada ya Musa kulikuwa na “manabii” wengine ambao pia waliandika vitabu vilivyovuviwa na Roho wa Mungu. Yoshua, kwa mfano, aliandika maneno yake katika “kitabu” kilichoitwa “torati ya Mungu” (Yos. 24:26) ili watu wapate kusikia “maneno yote ya BWANA aliyonena” kwa Yoshua (mst. 27); ingawa Yoshua alikiita kitabu chake “torati ya Mungu,” kama ambavyo wakati mwingine Agano la Kale kwa ujumla wake linarejelewa kama “Torati” (rej. Mt. 5:18; Yh. 15:25; Mdo

79

Made with FlippingBook Digital Publishing Software