Theology of the Church, Swahili Mentor Guide

/ 1 4 5

THEOLOJIA YA KANISA

ambacho Biblia inafundisha moja kwa moja kuhusu jukumu na kazi ya Kanisa? * Ni ipi njia bora zaidi ya sisi kufundisha vigezo na kanuni hizi kwa wengine ndani ya makusanyiko tunayotumikia? Je, ni muhimu kiasi gani kwetu kuwafundisha washirika wetu kwa msingi wa “Mapokeo Makuu,” mafundisho na mapokeo ya jamii pana ya Kikristo? * Je, baadhi ya vigezo na taswira za Kanisa na kazi zake zinafaha kutumiwa katika majiji zaidi kuliko vingine? Elezea. * Je, inawezekana, hata kwa kutumia vigezo na picha hizi, kutambua “kanisa la kweli” au “kusanyiko la kweli?” Ni ipi njia bora zaidi ya kutumia vigezo hivi katika kuwasaidia Wakristo na makusanyiko kukua katika mapenzi ya Mungu kwa maisha yao? * Je, kuna umuhimu gani wa Bwana kutupa picha nyingi sana za Kanisa katika Agano la Kale na Agano Jipya? Je, tunapaswa kutafuta kufanya nini katika kushughulika na picha nyingi sana za Kanisa – je zilikusudiwa kueleweka kwa kuhusianishwa kila moja na nyingine au kueleweka kila moja peke yake, au yote mawili? * Je, tunazitumiaje taswira hizi katika kuhubiri, kufundisha, na kufanya wanafunzi kwa namna ambayo inawapa wale tunaowaongoza picha bora zaidi ya Kanisa? Kusanyiko moja ambalo limeanzishwa kupitia mgawanyiko wa kanisa uliosababisha huzuni na maumivu mengi, linatatizika na uhusiano wake na makanisa mengine. Ingawa uongozi wake haujaacha kabisa wazo la kuwa na uhusiano na makanisa mengine kwa ajili ya ushirika na huduma, wanajali sana hitaji la kukuza kusanyiko lao jipya na kuleta utulivu wa washiriki wa kusanyiko hilo. Imekuwa zaidi ya miezi 10 tangu mgawanyiko huo ulipotokea, na katika muda huo wote hakujawa na tukio lolote ambapo kusanyiko hilo jipya lingeweza kukutana na Wakristo wengine kwa ajili ya ushirika na kujengana. Baadhi ya makusanyiko jirani yanaanza kutilia shaka uamuzi wa kiongozi wa kusanyiko jipya kuhusu hitaji la kuleta utulivu kwa kulitenga kanisa kutoka mbali na makusanyiko mengine. Je, vigezo na taswira tulizojifunza katika somo la juma hili zinahusiana vipi na changamoto hizi za kutaniko hili changa sasa? Je, wafanye nini kwa kuzingatia vigezo na picha tulizojifunza? Sisi Pekee

4

MIFANO

1

ukurasa 265  14

Made with FlippingBook - Share PDF online