Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa
12
Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa
mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu. 6 Tena akasema, Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akaficha uso wake; kwa maana aliogopa kumwangalia Mungu. 7 Bwana akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; 8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi. 9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. 10 Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.”
2 Kor. 4:6 Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang’aa toka gizani, ndiye aliyeng’aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo. Gal. 1:15-17 Lakini Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu, akaniita kwa neema yake, 16 alipoona vema kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili niwahubiri Mataifa habari zake; mara sikufanya shauri na watu wenye mwili na damu; 17 wala sikupanda kwenda Yerusalemu kwa hao waliokuwa mitume kabla yangu; bali nalikwenda zangu Arabuni, kisha nikarudi tena Dameski.
A. Wito wa kinabii wa Mungu: Mchungaji wa kondoo mwenye umri wa miaka 80, mwali wa moto katika kichaka kinachowaka, na shauku ya Mungu ya kuokoa watu kwa ajili yake mwenyewe (Kut. 3:2-10).
1. Ishara ya kujifunua: mwali wa moto kutoka kwenye kichaka, Kut. 3:2
2. Maelezo na maelekezo ya BWANA, Kut. 3:4
3. Mwitikio wa aliyeitwa, Kut. 3:4
4. Utambulisho wa Mungu kwa aliyeitwa, Kut. 3:5-6
5. Agizo la Mungu, Kut. 3:7-10
Kumbuka: muundo huu unarudiwa katika miito mingi ya kinabii katika Agano la Kale ([yaani, kutokewa, mjadala, mwitikio, ufunuo, agizo], rej. Mwa. 22:1-2, 11-12; 31:11-13; 46:2- 3; Kut 3:2-10; Gerhard Lohfink, The Conversion of St. Paul: Narrative and History in Acts . Chicago: Fransciscan Herald, 1976, uk. 61-69).
Made with FlippingBook Digital Publishing Software