Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa
Kipinidi cha 1 : Utangulizi
13
B. Tangu tamko la kwanza la Injili (proto-evangelium) hadi Yerusalemu Mpya: ulimwengu uko vitani, Mwa. 3:15; 1 Yoh. 3:8.
1. Msingi wa kito ni katika nafsi ya Mungu mwenyewe, Dan. 4:34-35 – Hata mwisho wa siku hizo, mimi, Nebukadreza, nikainua macho yangu kuelekea mbingu, fahamu zangu zikanirudia; nikamhimidi Yeye aliye juu, nikamsifu na kumheshimu Yeye aishiye milele; kwa maana mamlaka yake ni mamlaka ya milele, na ufalme wake hudumu toka kizazi hata kizazi; 35 na watu wote wanaokaa duniani wamehesabiwa kuwa si kitu, naye hufanya kama atakavyo, katika jeshi la mbinguni, na katika hao wanaokaa duniani; wala hapana awezaye kuuzuia mkono wake, wala kumwuliza, Unafanya nini wewe? a. BWANA kama Mwenye Enzi Kuu, Mungu wa Utatu: Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu; Zab. 83:18 (NEN) – Hebu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Bwana, kwamba wewe peke yako ndiwe Uliye Juu Sana ya dunia yote. b. BWANA Mungu kama Muumba na Aliyefanya vitu vyote; Zab. 24:1-2 – Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake. 2 Maana ameiweka misingi yake juu ya bahari, Na juu ya mito ya maji aliithibitisha.
2. Ibilisi na wanadamu katika uasi wa hiari dhidi ya utawala na mapenzi yake, walikaidi mapenzi makamilifu ya Mungu na meama yake (Mwa. 3:15).
3. Matokeo: machafuko ya laana, kuingia kwa uovu, kutengwa, na kifo (Rum. 3:23; 6:23).
4. Mapenzi ya Mungu ya ukombozi: kusimamisha tena utawala wa Ufalme wake katika ulimwengu wote.
Made with FlippingBook Digital Publishing Software