Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

14

Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa

a. Kushinda nguvu za uasi na machafuko (Kol. 2:15)

b. Kuurejesha upya uumbaji wake kwa utukufu wake (Isa. 43:7; Ufu. 4:11)

c. Kuwakomboa watu kwa ajili yake mwenyewe (Tit. 2:11-15)

d. Kufunua utukufu wake kupitia kwa Mwanawe na Kanisa (Efe. 1:13–14)

C. Umuhimu wa hadithi ya Kutoka kama kielelezo cha wito mmoja wa Mungu

1. Kama kielelezo cha kibiblia cha kuelewa vipengele vya wito wa Mungu

2. Kama taswira ya simulizi inayosaidia “kuhisi” nguvu ya wito

3. Kama mfano hai unaosaidia kuchambua na kuthamini wito wetu leo

4. Kama sehemu kiungo katika kazi endelevu ya Mungu kwa watu wake.

Maana yake “kuita, kutaja.” Mzizi huu unatokea katika Kiaramu cha Kale, Kikanaani, na Kiugariti, na lugha nyingine za Kisemiti (isipokuwa Kiethiopia). Neno hilo linaonekana katika vipindi vyote vya Kiebrania cha Biblia. Qara’ inaweza kumaanisha “utambulisho wa jina.” Kukipa kitu jina mara nyingi ni ishara ya mamlaka ya mtoa jina kwa kitu hicho, ambalo ndilo jambo la msingi katika matumizi ya kwanza ya qara’ : “Mungu akaiita nuru Mchana, na giza akaliita Usiku” (Mwa. 1:5). Tendo la Mungu la kuumba, “kutoa majina,” na kuhesabu hujumuisha nyota (Zab. 147:4) na vitu vingine

Made with FlippingBook Digital Publishing Software