Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa
Kipinidi cha 1 : Utangulizi
15
vyote (Isa. 40:26). Alimruhusu Adamu “kuwapa majina” wanyama kama udhihirisho thabiti wa mamlaka na ukuu wa mwanadamu juu ya wanyama (Mwa. 2:19). Ukuu na uteuzi wa kiungu umeenea kwa vizazi vyote, kwani Mungu “aliwaita” wote tangu mwanzo (Isa. 41:4; taz. Amo. 5:8). “Kumwita” au “kumtaja” mtu binafsi kunaweza kubainisha sifa kuu za mtu binafsi (Mwa. 27:36); kunaweza kuhusisha ungamo au tathmini (Isa. 58:13; Isa. 60:14); na kunaweza kuwa namna ya kutambua na kuutambulisha ukweli wa milele (Isa. 7:14). Kitenzi hiki pia kinatumika kuashiria “wito kwa kazi maalum.” Katika Kut. 2:7, Miriamu dadake Musa alimuuliza binti Farao kama aende “kumwita” (kumwagiza kutekeleza kazi) mlezi. Israeli “iliitwa” (kuchaguliwa) na Mungu kuwa watu wake (Isa. 65:12), kama ilivyokuwa kwa watu wa mataifa katika enzi ya Masihi (Isa. 55:5).
~ Vine’s Complete Expository Dictionary, Old Testament utafutaji-neno, toleo tepe katika programu ya kompyuta
D. Hadithi ya Kutoka kama hadithi ya vita: Yehova ni shujaa.
1. Yesu Kristo kama ashindaye ( Christus Victor) : Mwanakondoo ashindaye.
a. Ebr. 2:14 – Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi.
b. 1 Yoh. 3:5 – Nanyi mnajua ya kuwa yeye alidhihirishwa, ili aziondoe dhambi; na dhambi haimo ndani yake.
c. 1 Yoh. 3:8 – atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.
2. Watu wa agano la Mungu walihusika katika vita vya kiroho dhidi ya adui za Mungu.
Made with FlippingBook Digital Publishing Software