Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

126

Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme Wake Kupitia Kanisa

Mapokeo, mwendelezo

Ni vyema kutambua kwamba kila moja ya Mabaraza haya manne ya Kiekumene yalifanyika katika muktadha wa kitamaduni wa kabla wa Ulaya na kwamba hakuna hata moja lililofanyika huko Ulaya. Yalikuwa mabaraza ya Kanisa zima na yaliakisi wakati ambapo Ukristo ulikuwa dini ya mashariki katika msingi wake wa kijiografia. Kwa hesabu za kisasa, washiriki wake walikuwa Waafrika, Waasia, na Wazungu. Mabaraza yaliakisi kanisa ambalo “. . . lina mizizi katika tamaduni zilizo mbali sana na Ulaya na lililoutangulia utambulisho wa Ulaya ya sasa iliyoendelea, na [ambayo] baadhi ya watu wenye akili kubwa nyuma yake wamekuwa ni Waafrika” (Oden, The Living God, San Francisco: HarperSanFrancisco, 1987, p. 9). Pengine mafanikio muhimu zaidi ya Mabaraza yalikuwa kuundwa kwa kile kinachojulikana kwa kawaida Imani ya Nikea. Inatumika kama kauli ya muhtasari wa imani ya Kikristo ambayo inaweza kuafikiwa na Wakristo wa Kikatoliki, Waorthodoksi na Waprotestanti.

Mabaraza manne ya kwanza ya Kiekumene yamefupishwa katika chati ifuatayo:

Jina/Tarehe/Mahali

Kusudi

Kutetea dhidi ya: Uariani Swali lililojibiwa: Je, Yesu Alikuwa Mungu?

Baraza la Kwanza la Ekumeni 325 A.D. Nikea, Asia Ndogo Baraza la Pili la Ekumeni 381 A.D. Konstantinopoli, Asia Ndogo

Hatua: Uliundwa muundo wa awali wa Imani ya Nikea kutumika kama muhtasari wa imani ya Kikristo

Kutetea dhidi ya: Umakedonia Swali lililojibiwa: Je, Roho Mtakatifu ni ana sehemu sawa katika Uungu wa Mungu? Hatua: Kukamilishwa kwa Imani ya Nikea kwa kupanua makala inayohusu Roho Mtakatifu Kutetea dhidi ya: Unestori Swali lililojibiwa: Je, Yesu Kristo ni Mungu na mwanadamu katika nafsi moja? Hatua: Kumfafanua Kristo kuwa Neno la Mungu

Baraza la Tatu la Ekumeni 431 A.D. Efeso, Asia Ndogo

Aliyefanyika Mwili na kumthibitisha mama yake Mariamu kama theotokos (aliyembeba Mungu)

Kutetea dhidi ya: Monophysitism Swali lililojibiwa: Yesu anawezaje kuwa Mungu na mwanadamu? Hatua: Uhusiano kati ya asili mbili za Yesu (binadamu na Kimungu) ulielezwa

Baraza la Tatu la Ekumeni 451 A.D. Kalsedonia, Asia Ndogo

Made with FlippingBook Digital Publishing Software