Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa

Kipindi cha 3 : Wito wa Utakatifu

41

Dhana Potofu Iliyoenea

Kanusho la Kibiblia

Mungu huwaita wanaume tu wamtumikie

Euodia na Sintike, watenda kazi pamoja na Paulo (Flp. 4:2)

Watu wanaoitwa si watu wa kawaida kiroho

Hakuna aliye na uwezo ndani yake mwenyewe (2 Kor. 3:4-5)

Hitaji kuu ni mtu kuwa na haiba fulani ya uchangamfu

Mungu huchagua kwa msingi wa mapenzi yake, si haiba (2 Kor. 10:7). Baadhi humwagilia na kupanda, lakini Mungu ndiye anayekuza (1Kor. 3:6) Watu wasio na elimu wanaweza kupokea wito wa kitume (Mdo. 4:13)

Watu walioitwa wanawajibika kwa habari ya matunda

Elimu rasmi, iliyoidhinishwa na ya kitaaluma ni hitaji la lazima kwa wito maalum Ufasaha na uthabiti katika maneno ni muhimu kwa wito maalum Udhaifu endelevu unakukosesha sifa moja kwa moja

Nguvu za Mungu hushinda usemi mzuri (1 Kor. 2:1-5)

Wito wa Mungu, Warumi 11:29

Nguvu ya Kristo inakamilishwa katika udhaifu (2 Kor. 12:9-10)

Mungu wa nafasi ya pili (na ya ishirini na mbili) (Mdo. 15:35-40 pamoja na 2 Tim. 4:11)

Ukianguka tu, umetengwa milele

II. Kuitikia Wito

A. Matokeo yake kwa huduma ya mjini

1. Wewe si mali yako tena; Mungu ndiye Mmiliki wako na Msimamizi wako (utakatifu unahusu umiliki na kujitoa), Rum. 12:1-2 – Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. 2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software